logo spc.r_ad0
sp.b_ad0
blu.strip
spc.bt_blu.strip
HABARI MPYA KITAIFA DAR MIKOANI TAHARIRI MAKALA MICHEZO
sp.b_menu
ban
sp.b_ban
jumatatu, 11 septemba 2006
Pekua Tovuti
sp.t_sech.box sp.tafuta_w_tuma sp.t_tuma sp.r_tuma
sp.b_box sp.b_tuma
sp.b_F1
h.sep1
sp.r_men
sp.t
Gazeti la Jana
Matangazo
Bei zetu
Wasiliana nasi
Tuma habari
sp.b_tuma
sp.l_men
h.sep1
sp.l sp.t sp.r
LOGIN
sp.men.l sp.men.t sp.men.r
Username
sp.b_user
sp.t-word
Password
sp.b_word
sp.t_btn
sp.b_btn
sp.b
h.sep1
tp.spc

Wataalamu waaswa kuwa macho utapeli wa taaluma


na Charles Mullinda

WATALAAMU nchini wametakiwa kuwa macho na baadhi ya kampuni binafsi zinazotaka kutumia utaalamu wao kuombea fedha katika mashirika ya kimataifa.

Tahadhari hiyo imetolewa mwishoni mwa wiki na Dk. Abel Gibbe alipokuwa akizungumza katika Ofisi za Tanzania Daima, Dar es Salaam.

Dk. Gibbe ambaye anadai kutapeliwa na Kampuni ya ED-Consult (T) Ltd. ya jijini Dar es Salaam, alisema alifuatwa na watendaji watatu wa kampuni hiyo ambao walimtaka awape cheti cha maelezo yake binafsi (CV) ili wayatumie kushindania mradi wa kimataifa wenye thamani ya dola 100,000.

“Walinifuata nyumbani kwangu Mbezi, wakaniomba CV yangu, ati waitumie kushindania mradi wa kuendesha utafiti na kutoa mafunzo ya kuimarisha elimu katika programu ya Education II Project Zanzibar.

“Walidai mradi huo utafadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia African Development Bank, wakaniahidi kunilipa sh milioni 3 kila mwezi kwa vile mimi ndiye ningeendesha mradi huo, nikakubaliana nao, niliwapa CV yangu, na nimefanya kazi katika mradi huo, lakini wamenitapeli,” alilalamika Dk. Gibbe.

Alisema kwa kutumia CV yake, kampuni hiyo kwa kushirikiana na kampuni moja ya India ya Education Consultants India Ltd walifanikiwa kuupata mradi ambao ulianza kufanya kazi Oktoba 2000.

Alisema alifanya kazi Zanzibar kwa muda wa miezi saba kwa gharama zake baada ya Ed- Consult kutoa malalamiko ya mara kwa mara kwake kuwa haina fedha.

“Kwa muda wote niliofanya kazi Zanzibar walinipa sh 930,000 fedha nyingine wananizungusha wakati ninajua wamekwishalipwa.

“Hawa ni watu hatari, wametumia CV yangu na elimu yangu katika mradi wao, badala ya kunilipa stahili yangu wamenitapeli, wananizungusha, shida yao ilikuwa kunitumia kama chombo cha kupatia fedha kisha wanitelekeze.

“Kibaya zaidi, kwa sababu niliwaamini, nilitumia fedha zangu nyingi katika kukamilisha mradi huo, akiba yangu imebakia kidogo na nina familia inanitegemea, ninachanganyikiwa,” alisema Dk. Gibbe.

Alitoa tahadhari kwa wataalamu wengine kuwa makini na kampuni zinazoendesha mambo yake kiujanja janja kwa sababu zinaweza kuwaita na kutumia vyeti vyao katika njia mbaya au kuwatapeli.

 


h.sep

juu sp.b
Habari Mpya  |  Kitaifa  |  Dar  |  Mikoani  |  Tahariri  |  Makala  |  Michezo  |  Matangazo  |  Webmaster
Copyright 2006 © FreeMedia Ltd.
Free media limited
mtaa wa mkwepu na makunganya, slp 15261, dar es salaam, tanzania
simu +255-22-2120604  •  faksi +255-22-2126234