logo spc.r_ad0
sp.b_ad0
blu.strip
spc.bt_blu.strip
HABARI MPYA KITAIFA DAR MIKOANI TAHARIRI MAKALA MICHEZO
sp.b_menu
ban
sp.b_ban
jumanne, 12 septemba 2006
Pekua Tovuti
sp.t_sech.box sp.tafuta_w_tuma sp.t_tuma sp.r_tuma
sp.b_box sp.b_tuma
sp.b_F1
h.sep1
sp.r_men
sp.t
Gazeti la Jana
Matangazo
Bei zetu
Wasiliana nasi
Tuma habari
sp.b_tuma
sp.l_men
h.sep1
sp.l sp.t sp.r
LOGIN
sp.men.l sp.men.t sp.men.r
Username
sp.b_user
sp.t-word
Password
sp.b_word
sp.t_btn
sp.b_btn
sp.b
h.sep1
tp.spc

Vigogo Dodoma waongoza kuiibia DUWASA


Na Martha Mtangoo, Dodoma

VIGOGO mjini hapa ndio wanaoongoza kwa kuiibia maji Mamlaka ya Majisafi na Majitaka mjini Dodoma (DUWASA).

Hayo yamebainishwa juzi mjini hapa na Mkurugenzi wa mamlaka hiyo, Peter Mokiwa, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.

Alisema wafanyabiashara maarufu, wamiliki wa hoteli na vigogo serikalini ndio wanaoongoza kuiibia mamlaka hiyo kwa kujiunganishia maji kinyume cha sheria, jambo ambalo limekuwa likiiingizia mamlaka hiyo hasara kubwa.

Alisema kutokana na wizi huo, mamlaka hiyo imepata hasara ya sh milioni 53 katika kipindi cha kuanzia Januari 2005 hadi Juni 2006.

“Wamiliki wa hoteli, vigogo wanaofanya kazi serikalini na wafanyabiashara maarufu ndio wanaoongoza kwa kuiba maji na wanapokamatwa wanapatwa na shinikizo la damu na kuzirai,” alisema Mokiwa.

Pia mkurugenzi huyo alisema kutokana na watu hao kuambiwa wanatakiwa kulipa kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya faini ya kujiunganishia maji kinyume cha sheria, alisema sasa wameanzisha huduma ya kwanza kwa kuwa vigogo hao wamekuwa wakizirai baada ya kupewa taarifa ya kulipa fedha nyingi.

Mokiwa alisema watu wa kawaida ndio wanaoongoza kwa kulipa ankara za maji bila matatizo yoyote ikilinganishwa na watu wenye uwezo ambao hudhani kuwa kutokana na wadhifa walionao hawawezi kuchukuliwa hatua za kisheria

 


h.sep

juu sp.b
Habari Mpya  |  Kitaifa  |  Dar  |  Mikoani  |  Tahariri  |  Makala  |  Michezo  |  Matangazo  |  Webmaster
Copyright 2006 © FreeMedia Ltd.
Free media limited
mtaa wa mkwepu na makunganya, slp 15261, dar es salaam, tanzania
simu +255-22-2120604  •  faksi +255-22-2126234