logo spc.r_ad0
sp.b_ad0
blu.strip
spc.bt_blu.strip
HABARI MPYA KITAIFA DAR MIKOANI TAHARIRI MAKALA MICHEZO
sp.b_menu
ban
sp.b_ban
jumamosi, 10 Novemba 2007
Pekua Tovuti
sp.t_sech.box sp.tafuta_w_tuma sp.t_tuma sp.r_tuma
sp.b_box sp.b_tuma
sp.b_F1
h.sep1
sp.r_men
sp.t
Gazeti la Jana
Matangazo
Bei zetu
Wasiliana nasi
Tuma habari
sp.b_tuma
sp.l_men
h.sep1
sp.l sp.t sp.r
LOGIN
sp.men.l sp.men.t sp.men.r
Username
sp.b_user
sp.t-word
Password
sp.b_word
sp.t_btn
sp.b_btn
sp.b
h.sep1
tp.spc


Simba, Yanga zinatia aibu - Tenga
Awataka wanachama, viongozi kubadilika


na Khadija Kalili


RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodegar Chilla Tenga, amesema kitendo cha klabu kongwe za Simba na Yanga kugubikwa na migogoro, kinaitia aibu nchi.

Alisema jana jijini Dar es Salaam kwamba, kwa ukongwe wao, Simba na Yanga zilipaswa kuigwa kiuendeshaji na kimafanikio, lakini imekuwa kinyume cha hayo kwa kuendekeza migogoro isiyokwisha.

Tenga aliyewahi kukipiga katika klabu ya Pan Africans na timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, alisema migogoro hiyo imekuwa kikwazo cha maendeleo ya klabu hizo na soka kwa ujumla.

“Dunia nzima inajua katika soka ya Tanzania, kuna Simba na Yanga na hata viongozi wa CAF (Shirikisho la Soka la Afrika) na FIFA (Shirikisho la Soka la Kimataifa), wakija wanataka kuziona timu hizi,” alisema Tenga na kuongeza:
“Wanazo habari za ukongwe na upinzani wa jadi wa timu hizi, hivyo wafikapo, mbali na kuwa na hamu ya kuziona timu, hupenda kuzitembelea,” alisema.

Tenga alitoa mfano hai wa viongozi wa FIFA wanaokuja katika semina elekezi ya viongozi wa klabu za Ligi Kuu, itakayofanyika Jumatatu, Bagamoyo, Pwani, kwamba wameomba kuzitembelea klabu hizo.

“Jumanne, tutawapeleka viongozi wa FIFA katika klabu za Simba na Yanga, hivyo ni kitu cha aibu kukuta makufuli yakining’inia katika ofisi za Simba,” alisema.

Amezitaka Simba na Yanga kubadilika ili kwenda na wakati kwa kuiga mafanikio ya klabu nyingine zikiwamo za Afrika Magharibi na Kaskazini, ambazo kimafanikio zinalingana na zile za Ulaya.

Tenga aliyejitosa kuwania uwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) katika uchaguzi wa Desemba 7, alisema Simba na Yanga zibadilike.

Alisema, kubadilika ni kuanzia kwa wanachana na viongozi kwa ujumla sambamba na klabu husika kuwa na katiba bora zenye kuziba mianya ya mapinduzi.

Kauli hiyo imekuja huku uongozi wa kikatiba wa klabu ya Simba chini ya Hassan Dalali, ukiwa umesimamishwa na mkutano uliokuwa umepingwa na uongozi uliopo madarakani.

Tangu kusimamishwa kwa Dalali, ofisi za makao makuu ya klabu hizo, zimefungwa makufuli, moja la uongozi wa Dalali na jingine la wapinzani.

Kuhusu uwakilishi wa Simba katika semina hiyo ya Bagamoyo, Katibu Mkuu wa TFF, Frederick Mwakalebela, alisema majina yaliyowasilishwa kwao ni Makamu Mwenyekiti, Omar Gumbo, Katibu Msaidizi Mohammed Mjenga na Kocha Jamhuri Kihwelu.

Akigusia semina hiyo, Tenga alisema ina umuhimu mkubwa kwa soka la Tanzania na akazitaka klabu za Ligi Kuu kuitumia vema nafasi hiyo ya upendeleo.

Semina hiyo itafunguliwa na mkuu wa mafunzo kutoka FIFA, Jurg Nepfer kutoka Uswisi atakayewasili leo kwa ajili ya semina hiyo ambayo inafanyika katika nchi 10 tu kwa Afrika.

Tenga alisema suala la kutofautiana, ni kitu cha kawaida katika mchakato wa maendeleo, lakini tofauti hizo ziwe na hoja za msingi tofauti na ilivyo kwa Simba na Yanga.

Alisema kutokana na ukongwe na umaarufu wa Simba na Yanga, uimara na ufanisi wa klabu hizo, una faida kubwa kwa soka la Tanzania na kinyume chake, ni athari.


h.sep

juu sp.b
Habari Mpya  |  Kitaifa  |  Dar  |  Mikoani  |  Tahariri  |  Makala  |  Michezo  |  Matangazo  |  Webmaster
Copyright 2007 © FreeMedia Ltd.
Free media limited
mtaa wa Mkwepu na Makunganya, jengo la Bilicanas, gorofa ya kwanza, SLP 15261, Dar es salaam, Tanzania
simu +255-22-2126233  •  faksi +255-22-2126234  •  Selula  0713 296570