logo spc.r_ad0
sp.b_ad0
blu.strip
spc.bt_blu.strip
HABARI MPYA KITAIFA DAR MIKOANI TAHARIRI MAKALA MICHEZO
sp.b_menu
ban
sp.b_ban
jumatatu, 18 Juni 2007
Pekua Tovuti
sp.t_sech.box sp.tafuta_w_tuma sp.t_tuma sp.r_tuma
sp.b_box sp.b_tuma
sp.b_F1
h.sep1
sp.r_men
sp.t
Gazeti la Jana
Matangazo
Bei zetu
Wasiliana nasi
Tuma habari
sp.b_tuma
sp.l_men
h.sep1
sp.l sp.t sp.r
LOGIN
sp.men.l sp.men.t sp.men.r
Username
sp.b_user
sp.t-word
Password
sp.b_word
sp.t_btn
sp.b_btn
sp.b
h.sep1
tp.spc


Bakwata yatoa tuzo ya heshima


na Mobini Sarya


BARAZA Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA) limetoa tuzo za heshima kwa watu watano kutokana na mchango wao katika jamii.

Waliotunukiwa tuzo hizo ni Mkuu wa Vodacom Foundation, Rechal Phares, Mkrugenzi wa ITV na Radio One, Joyce Mhavile, Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB, Charles Kimei, mfanyabiashara Mustafa Sabodo na Mbunge wa Viti Maalum, Amina Chifupa (CCM). Hata hivyo, Amina hakuwapo wakati wa utoaji wa tuzo hizo.

Walitunikiwa tuzo hizo juzi na mke wa rais, Mama Salma Kikwete katika hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Tuzo hizo zilizopewa jina la Upendo wa Kweli, ni kwa ajili ya kuthamini mchango wa wahusika kwa jamii, hasa kusaidia vijana na watoto yatima.

Akizungumza baada ya kukabidhi tuzo hizo, Mama Salma, alisema: “Juni 16 tuliadhimnisha siku ya watoto kimataifa. Hii ni suku ambayo watu wote duniani tuliyakumbuka maandamano ya wanafunzi wa Soweto nchini Afrika Kusini. Mamia ya watoto waliuawa wakiwa wanadai haki zao pamoja na nchi yao.

“Mfuko wa Vodacom Foundation umekuwa ukihudumia watoto waishio katika mazingira magumu, walioathirika na virusi vya ukimwi kwa kugundua mahitaji yao na kuandaa mikakati madhubuti, ili kuwasaidia kwa kujitolea muda wao, misaada mbalimbali na kuwapatia vitu vya kuwawezesha.”

Phares aliishukuru Bakwata na Mama Kikwete kwa kugundua yote hayo na kuzithamini kazi nyingi zinazofanywa na Vodacom Foundation.

Hafla hiyo iliandaliwa na Bakwata kwa kushirikiana na Chama cha Kuendeleza Michezo na Kupambana na Ukimwi (TASCA).

Katika hafla hiyo, zilichangwa fedha taslimu sh milioni 55 na ahadi ilikuwa sh 118.9 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa shule ya watoto yatima inayojengwa na Bakwata kwa kushirikiana na TASCA.


h.sep

juu sp.b
Habari Mpya  |  Kitaifa  |  Dar  |  Mikoani  |  Tahariri  |  Makala  |  Michezo  |  Matangazo  |  Webmaster
Copyright 2007 © FreeMedia Ltd.
Free media limited
mtaa wa Mkwepu na Makunganya, jengo la Billicanas, gorofa ya kwanza, SLP 15261, Dar es salaam, Tanzania
simu +255-22-2126233  •  faksi +255-22-2126234  •  Selula  0713 296570