logo spc.r_ad0
sp.b_ad0
blu.strip
spc.bt_blu.strip
HABARI MPYA KITAIFA DAR MIKOANI TAHARIRI MAKALA MICHEZO
sp.b_menu
ban
sp.b_ban
jumatano, 20 Juni 2007
Pekua Tovuti
sp.t_sech.box sp.tafuta_w_tuma sp.t_tuma sp.r_tuma
sp.b_box sp.b_tuma
sp.b_F1
h.sep1
sp.r_men
sp.t
Gazeti la Jana
Matangazo
Bei zetu
Wasiliana nasi
Tuma habari
sp.b_tuma
sp.l_men
h.sep1
sp.l sp.t sp.r
LOGIN
sp.men.l sp.men.t sp.men.r
Username
sp.b_user
sp.t-word
Password
sp.b_word
sp.t_btn
sp.b_btn
sp.b
h.sep1
tp.spc


Ndesamburo atetea bia bungeni


na Rahel Chizoza, Dodoma


KATIKA hali ambayo haikutarajiwa, Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo (CHADEMA), ameitaka serikali kupunguza mara moja kodi katika bia.

Ndesamburo alitoa utetezi wake huo kwa bidhaa hiyo wakati akichangia bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2007/08 iliyowasilishwa wiki iliyopita na Waziri wa Fedha, Zakia Meghji.

Katika mchango wake, Ndesamburo alionyesha kusikitishwa na kitendo cha kodi ya bia kupanda kupitia bajeti ya mwaka 2007/08.

Mbunge huyo mkongwe na mfanyabiashara mzoefu, alitanabaisha kuwa kupanda kwa bei ya bia, kunaweza kusababisha wananchi waache kuinywa na kuhamia kwenye vilevi vingine ambavyo ni hatari kama vile gongo.

“Hivi kila mwaka mnaongeza bei kwenye bia tu hakuna vyanzo vingine vya mapato, mbona mnatuumiza jamani, au mnataka watoto wapate kwashakoo?” alihoji Ndesamburo.

Katika kauli iliyomaanisha jinsi watu wanavyothamini bia, Ndesamburo alisema ni vigumu kwa mtu kununua chakula cha mtoto au kulipa ada ya shule kabla hajatenga hela ya bia.

Aliitaka serikali kama ina nia ya watoto wasome, basi ipunguze kodi kwenye bia ili kuwawezesha wazazi kumudu gharama za vitu vingine.

“Mimi siwezi kuacha kunywa ka-bia kangu nimnunulie mtoto chakula, wote hapa tunakunywa bia jamani, tutaua watoto wetu na njaa, tupunguzieni,” aliomba Ndesamburo.

Alisema bia isipoongezwa kodi wananchi wataongeza kasi ya kunywa na kuiingizia serikali mapato zaidi kuliko ikiongezwa bei maana wanywaji watakuwa wachache.

Wakati huo huo, Ndesamburo ameshauri serikali ifunge migodi ya madini mpaka hapo itakapopata uwezo wa kuiendesha badala ya kuwaachia wageni waiendeshe.

Ndesamburo alisema kuwa chini ya utaratibu wa sasa, migodi mingi inawanufaisha zaidi wageni kuliko wenyeji ambao ndio wenye rasilimali.

Alisema haoni faida ya sekta ya madini katika uchumi wa nchi zaidi ya upotevu wa rasilimali za nchi ambazo zingeweza kutumiwa na watoto wa baadaye kwa masilahi ya taifa.

Alisema bajeti ya mwaka 2007/08 haiwezi kuleta maisha bora kwa kila Mtanzania kwa kutenga chini ya asilimia 10 ya bajeti kwa ajili ya sekta ya kilimo ambayo ndiyo inategemewa na wananchi wengi.

Alisema kiwango kilichotengwa kwa ajili ya kilimo hakitoshelezi mahitaji ya kilimo nchini na hakiwezi kuwaletea wananchi mapinduzi ya kilimo kwa haraka.

Aliulalamikia ukaguzi unaofanywa bandarini kwa wazalendo kuwa unadhalilisha utu wa mtu kwa kupekuliwa zaidi ya mara tano na watu tofauti.

Alisema hali hiyo inaonyesha Watanzania hawaaminiani, hali inayowatisha wageni kuja kufanya biashara zao Tanzania.

“Hivi sisi ni wezi kweli? Mnashindwa kuweka ukaguzi mmoja mpaka mtu akaguliwe na watu zaidi ya watano! Mnawatisha wawekezaji jamani,” alisema Ndesamburo.

Alisema Watanzania wanapaswa kuaminiana ili kuwashawishi wageni kuleta biashara zao na kuwavutia wawekezaji kuja kuwekeza ndani ya nchi.


h.sep

juu sp.b
Habari Mpya  |  Kitaifa  |  Dar  |  Mikoani  |  Tahariri  |  Makala  |  Michezo  |  Matangazo  |  Webmaster
Copyright 2007 © FreeMedia Ltd.
Free media limited
mtaa wa Mkwepu na Makunganya, jengo la Billicanas, gorofa ya kwanza, SLP 15261, Dar es salaam, Tanzania
simu +255-22-2126233  •  faksi +255-22-2126234  •  Selula  0713 296570