logo spc.r_ad0
sp.b_ad0
blu.strip
spc.bt_blu.strip
HABARI MPYA KITAIFA DAR MIKOANI TAHARIRI MAKALA MICHEZO
sp.b_menu
ban
sp.b_ban
jumatatu, 28 Januari 2008
Pekua Tovuti
sp.t_sech.box sp.tafuta_w_tuma sp.t_tuma sp.r_tuma
sp.b_box sp.b_tuma
sp.b_F1
h.sep1
sp.r_men
sp.t
Gazeti la Jana
Matangazo
Bei zetu
Wasiliana nasi
Tuma habari
sp.b_tuma
sp.l_men
h.sep1
sp.l sp.t sp.r
LOGIN
sp.men.l sp.men.t sp.men.r
Username
sp.b_user
sp.t-word
Password
sp.b_word
sp.t_btn
sp.b_btn
sp.b
h.sep1
tp.spc


TIC kupeleka wajasiriamali 67 Ujerumani


na Mwandishi Wetu


KITUO cha Uwekezaji nchini (TIC), kinatarajia kuwapeleka nchini Ujerumani wawekezaji wazalendo 67 kwa ajili ya kunadi miradi yao.

Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Emmanuel ole Naiko, alisema hayo mwishoni mwa wiki wakati wa hafla fupi ya kuuaga mwaka 2007 na kuukaribisha mwaka 2008 iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Alisema huo utakuwa ni mwendelezo wa mikakati ya kituo chake kilichojiwekea katika mwaka huu wa 2008, kuhakikisha kuwa kwa kufuata sheria ya nchi, wajasiriamali wazalendo wanaanza kumiliki uchumi wa miradi yao hapa nchini.

“Tunataka kufanya jinsi tuwezavyo kuwapeleka nje wawekezaji wa Kitanzania 67 nchini Ujerumani kwenda kunadi miradi yao,” alisema.

Hafla hiyo fupi iliwakutanisha wafanyakazi wa kituo na familia zao pamoja na wageni mbalimbali akiwepo Rais wa Shirikisho la wenye Viwanda, Biashara na Kilimo nchini (TCCIA), Alloyce Mwamanga.

Akizungumzia mafanikio waliyoyapata katika mwaka wa 2007, Ole Naiko, alisema kituo chake kimefanikiwa kuvuka karibu malengo yote waliyojiwekea.

Alisema awali kituo chake kilijiwekea mikakati ya kupata miradi 650, ambapo lengo lao limevuka kwa kupata miradi 701, hivyo wamevuka lengo kwa miradi 51.

Katika upande mwingine, Mkurugenzi huyo wa kituo cha uwewekezaji alisema mwaka 2007 kituo kilivuka lengo kwa asilimia 51 ambapo kilisajili miradi 701 badala 650 waliyojipangia.

“Tuliweza pia kushughulikia maombi 12,918, ukilinganisha na maombi 10,637 kwa mwaka 2006,” alisema na kuongeza kuwa kitengo cha kodi kilishughulikia maombi 4,984.


h.sep

juu sp.b
Habari Mpya  |  Kitaifa  |  Dar  |  Mikoani  |  Tahariri  |  Makala  |  Michezo  |  Matangazo  |  Webmaster
Copyright 2008 © FreeMedia Ltd.
Free media limited
mtaa wa Mkwepu na Makunganya, jengo la Bilicanas, gorofa ya kwanza, SLP 15261, Dar es salaam, Tanzania
simu +255-22-2126233  •  faksi +255-22-2126234  •  Selula  0713 296570