logo spc.r_ad0
sp.b_ad0
blu.strip
spc.bt_blu.strip
HABARI MPYA KITAIFA DAR MIKOANI TAHARIRI MAKALA MICHEZO
sp.b_menu
ban
sp.b_ban
jumatatu, 28 Januari 2008
Pekua Tovuti
sp.t_sech.box sp.tafuta_w_tuma sp.t_tuma sp.r_tuma
sp.b_box sp.b_tuma
sp.b_F1
h.sep1
sp.r_men
sp.t
Gazeti la Jana
Matangazo
Bei zetu
Wasiliana nasi
Tuma habari
sp.b_tuma
sp.l_men
h.sep1
sp.l sp.t sp.r
LOGIN
sp.men.l sp.men.t sp.men.r
Username
sp.b_user
sp.t-word
Password
sp.b_word
sp.t_btn
sp.b_btn
sp.b
h.sep1
tp.spc


Sheikh ashauri elimu sekondari iwe bure


na Mwandishi Wetu


MWENYEKITI wa Kamati ya Jumuiya ya Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Musa Kundecha, amesema ndoa za utotoni zitapungua au kwisha kabisa iwapo serikali itaweka sheria, sera na mipango itakayowezesha watoto wote wa kike na wa kiume kupata elimu bure angalau hadi kidato cha nne.

Alisema azma hiyo itafanikiwa iwapo pia serikali itaweka sheria kali na kusimamia kikamilifu utekelezaji wake, ili kuhakikisha kila atakayebainika kumpa mimba mtoto wa shule anaadhibiwa kikamilifu.

Sheikh Kundecha, alisema hayo mwishoni mwa wiki ofisini kwake Magomeni, Dar es Salaam katika mahojiano maalum na mwandishi wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA).

Alisema anaamini kukiwa na utaratibu wa kumwezesha kila mtoto wa kike na wa kiume kusoma bure angalao hadi kidato cha nne, kutapunguza au kuondoa kabisa tatizo la ndoa za utotoni nchini.

Kiongozi huyo wa dini, alisema hivi sasa wasichana wengi hasa wa familia maskini ndio wanaoathirika zaidi na tatizo la ndoa za utotoni kwa sababu wanapoishia darasa la saba au chini yake, wanakuwa hawana shughuli ya kufanya kwa manufaa yao, hivyo hushawishika au kulazimishwa kuolewa.

“Azma ya kutokomeza ndoa za utotoni nchini itafanikiwa kwa kiwango kikubwa iwapo pia kila mwanajamii atajiepusha na mambo yanayosababisha watoto wa kike kukatisha masomo,” alisema.


h.sep

juu sp.b
Habari Mpya  |  Kitaifa  |  Dar  |  Mikoani  |  Tahariri  |  Makala  |  Michezo  |  Matangazo  |  Webmaster
Copyright 2008 © FreeMedia Ltd.
Free media limited
mtaa wa Mkwepu na Makunganya, jengo la Bilicanas, gorofa ya kwanza, SLP 15261, Dar es salaam, Tanzania
simu +255-22-2126233  •  faksi +255-22-2126234  •  Selula  0713 296570