logo spc.r_ad0
sp.b_ad0
blu.strip
spc.bt_blu.strip
HABARI MPYA KITAIFA DAR MIKOANI TAHARIRI MAKALA MICHEZO
sp.b_menu
ban
sp.b_ban
ijumaa, 15 Februari 2008
Pekua Tovuti
sp.t_sech.box sp.tafuta_w_tuma sp.t_tuma sp.r_tuma
sp.b_box sp.b_tuma
sp.b_F1
h.sep1
sp.r_men
sp.t
Gazeti la Jana
Matangazo
Bei zetu
Wasiliana nasi
Tuma habari
sp.b_tuma
sp.l_men
h.sep1
tp.spc


Tandahimba wafuata mtandao Newala
MBUNGE JIMBO LA TANDAHIMBA


na Peter Nyanje na Rahel Chizoza, Dodoma


MBUNGE wa Tandahimba, Juma Njwayo (CCM), jana aliliambia Bunge kuwa, wakazi wa Wilaya ya Tandahimba mkoani Mtwara wanalazimika kusafiri masafa marefu kwenda Newala kufuata huduma za mtandao, EMS na fax kutokana na wilaya hiyo kutokuwa na ofisi za Shirika la Posta.

Alitoa taarifa hizo jana wakati akiuliza swali la nyongeza na kubainisha kuwa, huo umekuwa ni usumbufu mkubwa kwa wakazi wa wilaya hiyo, na kuiomba serikali kuangalia namna ya kulimaliza tatizo hilo.

Aliitaka serikali kuwaeleza wananchi wa wilaya hiyo ni lini Shirika la Posta litajenga ofisi yake ya kudumu wilayani humo, kwani hivi sasa inatumia kontena kama ofisi.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Dk. Maua Daftari, alisema ni kweli kuwa mji wa Tandahimba, ambao ni makao makuu ya Wilaya ya Tandahimba, hauna jengo rasmi kwa ajili ya huduma za Posta na badala yake kontena hutumika kwa madhumuni hayo.

Alisema hali kama hiyo ipo pia katika wilaya nyingine nchini, hasa zile mpya, kutokana na hali mbaya ya kifedha inayolikabili Shirika la Posta.

Hata hivyo, alisema baada ya serikali kufanya maamuzi yanayolenga kuliweka Shirika la Posta katika hali nzuri kifedha, shirika hilo litaanza kutekeleza mikakati yake ya kibishara ikiwa ni pamoja na kujenga majengo katika makao makuu ya wilaya.

Kutokana na mkakati huo, alisema Wilaya ya Tandahimba itajumuishwa na hadi hivi sasa tayari shirika hilo limeshakodi nyumba wilayani Tandahimba itakayotumika kama ofisi ya Posta baada ya matengenezo.


h.sep

juu sp.b
Habari Mpya  |  Kitaifa  |  Dar  |  Mikoani  |  Tahariri  |  Makala  |  Michezo  |  Matangazo  |  Webmaster
Copyright 2008 © FreeMedia Ltd.
Free media limited
mtaa wa Mkwepu na Makunganya, jengo la Bilicanas, gorofa ya kwanza, SLP 15261, Dar es salaam, Tanzania
simu +255-22-2126233  •  faksi +255-22-2126234  •  Selula  0713 296570