logo spc.r_ad0
sp.b_ad0
blu.strip
spc.bt_blu.strip
HABARI MPYA KITAIFA DAR MIKOANI TAHARIRI MAKALA MICHEZO
sp.b_menu
ban
sp.b_ban
ijumaa, 15 Februari 2008
Pekua Tovuti
sp.t_sech.box sp.tafuta_w_tuma sp.t_tuma sp.r_tuma
sp.b_box sp.b_tuma
sp.b_F1
h.sep1
sp.r_men
sp.t
Gazeti la Jana
Matangazo
Bei zetu
Wasiliana nasi
Tuma habari
sp.b_tuma
sp.l_men
h.sep1
tp.spc


CUF wadai kubaini udanganyifu daftari la wapiga kura


na Asha Bani


CHAMA cha Wananchi (CUF), kimedai kubaini udanganyifu kwenye maboresho ya daftari la wapiga kura, zoezi ambalo limemalizika mwishoni mwa wiki katika Mkoa wa Ruvuma.

Hayo yamebainishwa juzi na Ofisa wa Sera wa CUF, Hussein Mmasi, alipozungumza na Tanzania Daima ofisini kwake Buguruni, Dar es Salaam.

Alisema udanganyifu huo umebainika baada ya chama hicho kupata malalamiko mbalimbali kutoka kwa baadhi ya wananchi katika vituo mbalimbali ambavyo vilitumika kuandikisha kura wakati wa Uchaguzi Mkuu mwaka 2005.

Mmasi alivitaja vituo hivyo ikiwa ni pamoja na kuainisha baadhi ya udanganyifu ambao wananchi waliuwekea wasiwasi kuwa ni pamoja na kituo cha Tarafani, Majengo na Muungano.

Alisema katika vituo hivyo kulitokea mtafaruku baada ya mtu mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Omari katika kituo cha Muungano alikuwa akipita na kukusanya shahada za watu na kuanza kunakili namba, kitendo ambacho hakikutakiwa.

“Baada ya wananchi kubaini hivyo baadhi walimkamata na kumpeleka katika kituo kidogo cha polisi ambapo alidai baada ya muda mfupi aliachiwa,” alisema.

Alisema mbali na hilo katika kituo kilichopo Shule ya Mtina, mwandikishaji alikuwa anatumia daftari kama za wanafunzi kuhakiki na kuwa wamekamata baadhi ya vitambulisho ambavyo vilikuwa na tofauti na vile vya awali.

“Vitambulisho hivyo vilikuwa na tofauti kubwa kutokana na kuwa havina anwani, kata ya mtu alikotoka, kijiji wala mkoa,” alisema Mmasi.

Alisema tayari amezungumza na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Rajabu Kiravu, ambaye alimuahidi kufuatilia suala hilo.

Akizungumza na Tanzania Daima kuhusu hilo, Kiravu alikiri kupata malalamiko hayo, lakini alipoyafanyia kazi alibaini kuwa hayakuwa na ukweli.


h.sep

juu sp.b
Habari Mpya  |  Kitaifa  |  Dar  |  Mikoani  |  Tahariri  |  Makala  |  Michezo  |  Matangazo  |  Webmaster
Copyright 2008 © FreeMedia Ltd.
Free media limited
mtaa wa Mkwepu na Makunganya, jengo la Bilicanas, gorofa ya kwanza, SLP 15261, Dar es salaam, Tanzania
simu +255-22-2126233  •  faksi +255-22-2126234  •  Selula  0713 296570