logo spc.r_ad0
sp.b_ad0
blu.strip
spc.bt_blu.strip
HABARI MPYA KITAIFA DAR MIKOANI TAHARIRI MAKALA MICHEZO
sp.b_menu
ban
sp.b_ban
ijumaa, 15 Februari 2008
Pekua Tovuti
sp.t_sech.box sp.tafuta_w_tuma sp.t_tuma sp.r_tuma
sp.b_box sp.b_tuma
sp.b_F1
h.sep1
sp.r_men
sp.t
Gazeti la Jana
Matangazo
Bei zetu
Wasiliana nasi
Tuma habari
sp.b_tuma
sp.l_men
h.sep1
tp.spc


AY awa wakala wa muziki Afrika Mashariki


na Khadija Kalili


MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Ambwene Yesayah ‘AY’, amefungua kampuni ya uwakala wa wasanii wa nchi za Afrika Mashariki katika mabara ya Asia, Ulaya na Amerika.

Akizungumza na Tanzania Daima, AY amesema lengo la kuwa wakala ni kukuza na kuinua vipaji vya wasanii chipukizi na wale wenye muda mrefu katika muziki huo wa kizazi kipya katika nchi za Kenya, Tanzania na Uganda.

Aidha, kampuni hiyo itakuwa ikijishughulisha na matangazo ya biashara kwa wasanii yanayohusu masuala ya burudani.

AY anakuwa msanii wa kwanza kuwa wakala kwa lengo la kutaka kuwaendeleza wasanii wa Afrika Mashariki.

Kabla ya hapo pia msanii huyo mwishoni mwa mwaka jana alizindua mavazi yenye nembo yake.


h.sep

juu sp.b
Habari Mpya  |  Kitaifa  |  Dar  |  Mikoani  |  Tahariri  |  Makala  |  Michezo  |  Matangazo  |  Webmaster
Copyright 2008 © FreeMedia Ltd.
Free media limited
mtaa wa Mkwepu na Makunganya, jengo la Bilicanas, gorofa ya kwanza, SLP 15261, Dar es salaam, Tanzania
simu +255-22-2126233  •  faksi +255-22-2126234  •  Selula  0713 296570