logo spc.r_ad0
sp.b_ad0
blu.strip
spc.bt_blu.strip
HABARI MPYA KITAIFA DAR MIKOANI TAHARIRI MAKALA MICHEZO
sp.b_menu
ban
sp.b_ban
jumamosi, 16 Februari 2008
Pekua Tovuti
sp.t_sech.box sp.tafuta_w_tuma sp.t_tuma sp.r_tuma
sp.b_box sp.b_tuma
sp.b_F1
h.sep1
sp.r_men
sp.t
Gazeti la Jana
Matangazo
Bei zetu
Wasiliana nasi
Tuma habari
sp.b_tuma
sp.l_men
h.sep1
tp.spc


Mvua yaharibu nyumba 33 Dar


na Safina Tibanyendela


NYUMBA 33 zimeezuliwa mapaa kutokana na mvua iliyonyesha juzi katika Kata ya Kizinga Mbagala, Dar es Salaam.

Akizungumza na Tanzania Daima juzi, mmoja wa wakazi wa eneo hilo, Ernest Nyambo, alisema mvua hiyo iliyoanza kunyesha saa 9 alasiri na kuendelea hadi saa 9.45 usiku, huku ikiandamana na upepo mkali iliezua mapaa ya nyumba hizo.

“Hatujaelewa kama ni kimbunga au ni nini…mvua ilikuwa ni kubwa mno na mara ukaja upepo mkali ulioezua mapaa ya nyumba na watu kulazimika kujihifadhi katika nyumba za jirani zao zilizosalimika,” alisema na kuongeza kuwa hakuna mtu aliyejeruhiwa.

Ofisa Mtendaji wa kata hiyo ameorodhesha majina ya watu wote walioathirika ili waweze kusaidiwa na kujua thamani yake.

Nyambo alisema pia kuwa mvua hiyo iliangusha ukuta wa kiwanda cha kutengeneza kanga cha Karibu Textile Mill uliojengwa hivi karibuni na kusababisha maji machafu kutoka kiwandani hapo kutiririkia katika makazi ya watu.

Hivyo, ameiomba serikali kuwasaidia ili waweze kuezeka nyumba zao, kwani wengi wao kipato chao ni duni.


h.sep

juu sp.b
Habari Mpya  |  Kitaifa  |  Dar  |  Mikoani  |  Tahariri  |  Makala  |  Michezo  |  Matangazo  |  Webmaster
Copyright 2008 © FreeMedia Ltd.
Free media limited
mtaa wa Mkwepu na Makunganya, jengo la Bilicanas, gorofa ya kwanza, SLP 15261, Dar es salaam, Tanzania
simu +255-22-2126233  •  faksi +255-22-2126234  •  Selula  0713 296570