MICHUANO ya soka na netiboli itakayojulikana kama Media Cup inatarajiwa kutimua vumbi kuanzia Machi mosi hadi 15 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Michuano hiyo ambayo itashirikisha vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini, imeandaliwa na Mfuko wa Hifadhi ya Taifa (NSSF).
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Juma Kintu, kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, mashindano ya mwaka huu yamezidi kuboreshwa ambako mbali ya soka, yatashirikisha pia netiboli.
Kintu alisema kuwa, vyombo mbalimbali vya habari vimepewa mwaliko na vinatakiwa kuthibitisha si zaidi ya kesho mchana.
Alivishukuru vyombo mbalimbali vya habari kwa ushirikiano wao na kuvitaka kuuendeleza.