logo spc.r_ad0
sp.b_ad0
blu.strip
spc.bt_blu.strip
HABARI MPYA KITAIFA DAR MIKOANI TAHARIRI MAKALA MICHEZO
sp.b_menu
ban
sp.b_ban
jumamosi, 16 Februari 2008
Pekua Tovuti
sp.t_sech.box sp.tafuta_w_tuma sp.t_tuma sp.r_tuma
sp.b_box sp.b_tuma
sp.b_F1
h.sep1
sp.r_men
sp.t
Gazeti la Jana
Matangazo
Bei zetu
Wasiliana nasi
Tuma habari
sp.b_tuma
sp.l_men
h.sep1
tp.spc


Simuhitaji Jokha Kassim - Yussuf


na Abdallah Menssah


KUNDI la taarab la Jahazi Modern, limekanusha uvumi ulioenea kwa kasi katika baadhi ya mitaa ya Jiji la Dar es Salaam, kuwa wana mpango wa kumnyakua Jokha Kassim wa Zanzibar Stars.

Mkurugenzi wa kundi hilo linalotumia mtindo wa ‘Nakshi Nakshi’, Mzee Yussuf ‘Mfalme’, alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa, habari hizo hazina ukweli wowote na kuwataka mashabiki wao kutotilia maanani.

“Naomba wapenzi na mashabiki wetu wote walioathirika na uzushi huo kupuuza taarifa hizo na naeleza bayana kuwa, sisi kama Jahazi, katakata hatumwitaji Jokha,” alisema Yussuf aliye mpapasa kinanda mahiri kwa upande wa taarab hapa nchini.

Yusssuf alisema kuwa, anaamini waimbaji alionao ndani ya kundi lake wanatosha, hivyo hakuna sababu ya msingi ya kumuongeza mwimbaji huyo licha ya uwezo wake wa kufanya kazi.

Uvumi wa kwamba Jahazi wana mpango wa kumchukua Jokha umezuka baada ya kuonekana mara kwa mara katika maonyesho ya Jahazi, ambako huingia na kuanza kucheza kwa ushabiki sambamba na kutunza baadhi ya waimbaji.


h.sep

juu sp.b
Habari Mpya  |  Kitaifa  |  Dar  |  Mikoani  |  Tahariri  |  Makala  |  Michezo  |  Matangazo  |  Webmaster
Copyright 2008 © FreeMedia Ltd.
Free media limited
mtaa wa Mkwepu na Makunganya, jengo la Bilicanas, gorofa ya kwanza, SLP 15261, Dar es salaam, Tanzania
simu +255-22-2126233  •  faksi +255-22-2126234  •  Selula  0713 296570