logo spc.r_ad0
sp.b_ad0
blu.strip
spc.bt_blu.strip
HABARI MPYA KITAIFA DAR MIKOANI TAHARIRI MAKALA MICHEZO
sp.b_menu
ban
sp.b_ban
jumatatu, 11 septemba 2006
Pekua Tovuti
sp.t_sech.box sp.tafuta_w_tuma sp.t_tuma sp.r_tuma
sp.b_box sp.b_tuma
sp.b_F1
h.sep1
sp.r_men
sp.t
Gazeti la Jana
Matangazo
Bei zetu
Wasiliana nasi
Tuma habari
sp.b_tuma
sp.l_men
h.sep1
sp.l sp.t sp.r
LOGIN
sp.men.l sp.men.t sp.men.r
Username
sp.b_user
sp.t-word
Password
sp.b_word
sp.t_btn
sp.b_btn
sp.b
h.sep1
tp.spc

Lowassa ajionea madini yanayotafunwa na wageni


na Charles Mullinda

KIGUGUMIZI cha serikali kuwabana wawekezaji kuanzisha viwanda vya kuchonga na kuongeza thamani ya madini nchini, kinalikosesha taifa mabilioni ya shilingi.

Waziri Mkuu, Edward Lowassa, akizungumza na waandishi wa habari jana katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere muda mfupi baada ya kuwasili nchini akitokea nchini Vietnam, alisema maelfu ya watu Thailand wanakata madini yanayotoka Tanzania.

“Thailand tumeona utaalamu wa kutengeneza vito, wale ni mabingwa wa kutengeneza vito, kuna madini ya tanzanite, yapo yanayopatikana

Tunduru na Songea, yanasafishwa na kuongezewa thamani tayari kwa kuuzwa.

“Ni jambo la kushangaza, wana viwanda vikubwa vya vito ambavyo madini wanayoshughulika nayo yanapatikana hapa nyumbani, kiwanda nilichoona kimeajiri watu 2,000.

“Tumewaomba waje waanzishe viwanda hivyo hapa nyumbani, pia tumewaomba wafundishe watu wetu utaalamu huo na wamekubali kufundisha watu wawili au watatu kwa mwaka.

“Lakini pia tumemuomba Waziri Msabaha abaki kuona kuna nini, vipi madini yetu yako kwa wingi kule na namna tunavyoweza kufaidika na utalaamu wa wenzetu pamoja na kufikia makubaliano mengine ya msingi katika sekta hii,” alisema Lowassa.

Kwa wenye kumbukumbu, hii si mara ya kwanza kwa Dk. Msabaha kubaki eneo hilo kwa lengo la ‘kujifunza’. Ameshajifunza mara nyingi, lakini kinachokwamisha, ni ahadi ambazo hazizai matunda.

Serikali ilishaahidi kuwa ingepiga marufuku usafirishaji wa madini ghafi miaka mitatu iliyopita. Hakuna kilichofanyika hadi sasa.

Akizungumzia mapinduzi ya kilimo yaliyofikiwa na Thailand, alisema nchi hiyo imepiga hatua kubwa kutokana na kutumia kilimo cha kisasa.

Alitoa mfano wa zao la muhogo ambalo pia linalimwa hapa nchini, kwamba Thailand linazalishwa kwa wingi kwa kutumia kilimo cha kisasa na kuuzwa China ambako muhogo unatumika kutengeneza mafuta mbadala.

“Kiteknolojia wenzetu wako juu, tumewaomba wailete teknolojia yao hapa kwetu, wana trekta lenye uwezo wa kupanda mpunga ekari moja kwa saa moja, trekta hili si aghali sana, tunaweza kununua kwa ajili ya wakulima wetu.

“Kwa ujumla wamepiga hatua kubwa ya maendeleo vijijini, wao wameanza zamani kupeleka vijijini dola 7,000, huko wananchi ndio wanaamua wafanye nini na fedha hizo,” alisema Lowassa.

Akizungumzia ziara yake nchini Vietnam, alisema ingawa nchi hiyo imepigana vita miaka 30, imeweza kupiga hatua kubwa kimaendeleo kwa muda mfupi na kufanikiwa kukuza uchumi wake.

Vietnam ni ya pili duniani kwa uzalishaji wa mazao ya mpunga, korosho na kahawa.

 


h.sep

juu sp.b
Habari Mpya  |  Kitaifa  |  Dar  |  Mikoani  |  Tahariri  |  Makala  |  Michezo  |  Matangazo  |  Webmaster
Copyright 2006 © FreeMedia Ltd.
Free media limited
mtaa wa mkwepu na makunganya, slp 15261, dar es salaam, tanzania
simu +255-22-2120604  •  faksi +255-22-2126234