logo spc.r_ad0
sp.b_ad0
blu.strip
spc.bt_blu.strip
HABARI MPYA KITAIFA DAR MIKOANI TAHARIRI MAKALA MICHEZO
sp.b_menu
ban
sp.b_ban
jumatatu, 11 septemba 2006
Pekua Tovuti
sp.t_sech.box sp.tafuta_w_tuma sp.t_tuma sp.r_tuma
sp.b_box sp.b_tuma
sp.b_F1
h.sep1
sp.r_men
sp.t
Gazeti la Jana
Matangazo
Bei zetu
Wasiliana nasi
Tuma habari
sp.b_tuma
sp.l_men
h.sep1
sp.l sp.t sp.r
LOGIN
sp.men.l sp.men.t sp.men.r
Username
sp.b_user
sp.t-word
Password
sp.b_word
sp.t_btn
sp.b_btn
sp.b
h.sep1
tp.spc

Wafugaji Meatu walalamika kubambikiziwa kesi


Na Asha Bani, aliyekuwa Meatu

JAMII ya wafugaji wa Wilaya ya Meatu, mkoani Shinyanga wamedai kuwa baadhi ya askari huwabambikizia kesi, ili kujipatia rushwa ya mifugo pamoja na fedha.

Wakizungumza na Tanzania Daima kwa nyakati tofauti, mmoja wa wanakijiji hao, Lucas Masanja alisema kuwa mara nyingi askari wa kijijini hapo huwa wanawabambikizia kesi ili kujipatia rushwa ya fedha na mifugo.

Mbunge wa jimbo hilo, Salum Khamis, alithibitisha kuwapo kwa tatizo hilo na kuahidi kulishughulikia kwa kushirikiana na mkuu wa polisi.

Khamis alisema kumekuwapo na malalamiko mengi ya wananchi kubambikiziwa kesi na kuongeza kuwa, lililomsikitisha zaidi ni lile la mzee wa kijijini hapo kubambikiziwa kesi ya mauaji ya binti yake, ambaye alifia hospitalini.

Alisema kuwa mzee huyo alibambikiwa kesi hiyo na Mkuu wa Polisi katika Kituo cha Meatu na kudai kuwa alimuua mtoto wake kwa kumpiga na fimbo.

“Binti wa mzee huyo alikuwa na ujauzito na alikuwa anaugua malaria kwa muda mrefu na baada ya kumpeleka hospitali alifariki dunia. Baba wa binti huyo alienda na kuuchukua mwili wa marehemu na kurudi nao nyumbani kuzika,” alisema mbunge huyo.

Alisema polisi baada ya kujua hilo, walikwenda nyumbani kwa mzee huyo na kumwamuru awapeleke kwenye kaburi ili kufukua na kuona kama marehemu ana majeraha ya fimbo ambayo wanadai kuwa ndiyo yaliyomsababishia kifo hicho.

“Ilipofukiliwa maiti ile, askari wale walisema kuwa ilikuwa na majeraha na ndipo walipomkamata mzee huyo na kumfungulia mashitaka hayo,” alisema.

 


h.sep

juu sp.b
Habari Mpya  |  Kitaifa  |  Dar  |  Mikoani  |  Tahariri  |  Makala  |  Michezo  |  Matangazo  |  Webmaster
Copyright 2006 © FreeMedia Ltd.
Free media limited
mtaa wa mkwepu na makunganya, slp 15261, dar es salaam, tanzania
simu +255-22-2120604  •  faksi +255-22-2126234