logo spc.r_ad0
sp.b_ad0
blu.strip
spc.bt_blu.strip
HABARI MPYA KITAIFA DAR MIKOANI TAHARIRI MAKALA MICHEZO
sp.b_menu
ban
sp.b_ban
jumamosi, 15 Desemba 2007
Pekua Tovuti
sp.t_sech.box sp.tafuta_w_tuma sp.t_tuma sp.r_tuma
sp.b_box sp.b_tuma
sp.b_F1
h.sep1
sp.r_men
sp.t
Gazeti la Jana
Matangazo
Bei zetu
Wasiliana nasi
Tuma habari
sp.b_tuma
sp.l_men
h.sep1
sp.l sp.t sp.r
LOGIN
sp.men.l sp.men.t sp.men.r
Username
sp.b_user
sp.t-word
Password
sp.b_word
sp.t_btn
sp.b_btn
sp.b
h.sep1
tp.spc


Wanafunzi IMTU waandamana kudai mikopo


na Agnes Mlundachuma


WAKATI serikali ikilalamikia upungufu wa madaktari nchini, baadhi ya wasomi wa mwaka wa kwanza wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Tiba na Teknolojia (IMTU), wamesimamishwa masomo baada ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu kushindwa kuwakopesha fedha za kulipia ada.

Kusimamishwa masomo kwa wanafunzi hao kuliwalazimu kuandamana hadi Wizara ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknoknlojia ili kujua hatma ya fedha za mikopo walizoahidiwa na serikali.

Jumla ya wanafumzi 137 walifika katika ofisi za wizara hiyo ili kutoa malalamiko yao.

Akizungumza kwa niaba ya wanafunzi wenzake, Biseko Mlebo alisema wameshangazwa na hatua ya Bodi ya Mikopo kuwataarifu kwa barua kwamba watapewa mikopo kwa kiasi kisichozidi sh milioni 2.6 huku kiasi kinachobaki kufika sh milioni sita wakitakiwa kujilipia.

Alisema, suala hilo limewashitua kwa vile walisaini katika bodi hiyo kwa madhumuni ya kupewa mkopo wa sh milioni sita ikiwa ni ada ya masomo kwa mwaka katika chuo hicho.

Mlebo, alisema barua hiyo imezima ndoto za watoto wa maskini wanaohitaji kusoma ili kupunguza matatizo ya afya vijijini.

Alisema, tatizo la upungufu wa madaktari limelalamikiwa na madaktari wenyewe wakati wa mkutano wao wa 41 uliomalizika hivi karibuni uliobainisha kuwa Tanzania ni nchi ya mwisho duniani kwa uhaba wa madaktari.

Pamoja na idadi hiyo ndogo, madaktari wanakimbilia nje ya nchi kutokana na maslahi kidogo ikilinganishwa na nchi nyingine.


h.sep

juu sp.b
Habari Mpya  |  Kitaifa  |  Dar  |  Mikoani  |  Tahariri  |  Makala  |  Michezo  |  Matangazo  |  Webmaster
Copyright 2007 © FreeMedia Ltd.
Free media limited
mtaa wa Mkwepu na Makunganya, jengo la Bilicanas, gorofa ya kwanza, SLP 15261, Dar es salaam, Tanzania
simu +255-22-2126233  •  faksi +255-22-2126234  •  Selula  0713 296570