MBUNGE wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela (CCM), ameitahadharisha serikali kuwa mpango wake mpya ilioubuni wa kupitisha mizigo na bidhaa za wawekezaji bandarini bila ya kukaguliwa, ni hatari kwa taifa...
JUZI wabunge wa kambi ya upinzani waliwasilisha kile walichokielezea kuwa ni bajeti mbadala iliyokuwa ikijibu hotuba ya bajeti ya Waziri wa Fedha, Zakia Meghji aliyoitoa Alhamisi ya wiki iliyopita. Wabunge hao wa upinzani katika mapendekezo yao hayo waliitaka serikali kuitengea sekta ya miundombinu kiwango kikubwa zaidi cha fedha kinachozidi asilimia 20 ya bajeti nzima...
WATANZANIA tuna kila sababu ya kusikia raha na furaha, sababu ya kujivuna na kujivunia, sababu ya kutembea vifua mbele na vichwa juu!
Ushindi wa timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, umetufanya si tu kujisikia wamoja, bali pia kujiona wamoja, kwani ushindi wao ni ushindi wa Tanzania...
SERIKALI haina mpango wa kulitangaza Jeshi la Mgambo kuwa sehemu ya jeshi kamili, Bunge limeelezwa jana. Akijibu swali la Mbunge wa Mpanda Kati, Said Amour Arfi (CHADEMA), aliyetaka kujua jeshi hilo litatambulika lini kama jeshi kamili...
WANAFUNZI tisa kati ya 12 wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), waliofukuzwa chuoni hapo kwa madai ya kuchochea mgomo, wamerejeshwa. Rais wa Serikali ya wanafunzi (IFM-SO), Boniphace Baltazar, alisema kurejea kwa wanafunzi hao tisa kumetokana na agizo la Waziri wa Fedha, Zakia Meghji, alilolitoa kwa uongozi huo juzi jioni...
KATIKA hali ambayo haikutarajiwa, Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo (CHADEMA), ameitaka serikali kupunguza mara moja kodi katika bia. Ndesamburo alitoa utetezi wake huo kwa bidhaa hiyo wakati akichangia bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2007/08 iliyowasilishwa wiki iliyopita na Waziri wa Fedha, Zakia Meghji...
KITUO cha British Council, leo kinatarajiwa kutoa maelezo jinsi wasanii wa Tanzania watakavyoweza kushiriki katika mpango wa kuwasaidia utakaofanyika nchini Uingereza hivi karibuni. Mpango huo unaojulikana kama ‘Bring Noise’, una lengo la kuboresha vipaji vya wanamuziki na wasanii...
NEEMA imezidi kuwashukia wachezaji wa timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, baada ya Benki ya National Microfinance (NMB), nayo jana kuwamwagia sh mil. 17. Huu ni mwendelezo wa neema kwa timu hiyo iliyowasili jijini Mwanza Jumapili usiku ikitokea Burkina Faso na kutua Dar es Salaam juzi jioni...