logo spc.r_ad0
sp.b_ad0
blu.strip
spc.bt_blu.strip
HABARI MPYA KITAIFA DAR MIKOANI TAHARIRI MAKALA MICHEZO
sp.b_menu
ban
sp.b_ban
alhamis, 14 Februari 2008
Pekua Tovuti
sp.t_sech.box sp.tafuta_w_tuma sp.t_tuma sp.r_tuma
sp.b_box sp.b_tuma
sp.b_F1
h.sep1
sp.r_men
sp.t
Gazeti la Jana
Matangazo
Bei zetu
Wasiliana nasi
Tuma habari
sp.b_tuma
sp.l_men
h.sep1
tp.spc


Zorro kuwapa raha wapendanao Dom


na Eugenia Kimolo


MWANAMUZIKI mahiri wa muziki wa kizazi kipya, Banana Zorro, akiwa na bendi yake ya B Band, amewaahidi wapendanao, kuwapa burudani ya aina yake katika onyesho litalorindima Siku ya Wapendanao ‘Valentine’s Day’, Februari 14 kwenye Ukumbi wa Royal Village mkoani Dodoma.

Akizungumza jana kwa simu, Zorro alisema kuwa yeye pamoja na bendi yake wamejichimbia kambini kwa ajili ya kujifua ili kutoa burudani ya aina yake siku hiyo.

Zorro alisema kuwa, anawaahidi wapendanao na wakazi wa mkoa huo na wa jirani burudani ya aina yake, kwani siku hiyo atatumia muda muafaka kuwaonjesha nyimbo mpya ambazo siku hiyo itakuwa ni mara ya kwanza kusikika.

“Nawaomba mashabiki na wapenzi wa muziki wa kizazi kipya, wafike kwa wingi kujipatia burudani ya nguvu kutoka kwetu maana siku hii ni muhimu na ndiyo maana na sisi tunawapenda,” alisema Zorro.

Zorro aliwataka wapenzi wa muziki wa kizazi kipya kujitokeza kwa wingi kupata burudani, vikiwamo vibao vinavyotamba sasa kama ‘Sultan', ‘Dar es Salaam’ aliomshirikisha Chai Jaba, pamoja na ‘Sikuhitaji Wewe’ aliomshirikisha Mwasiti na nyinginezo nyingi.


h.sep

juu sp.b
Habari Mpya  |  Kitaifa  |  Dar  |  Mikoani  |  Tahariri  |  Makala  |  Michezo  |  Matangazo  |  Webmaster
Copyright 2008 © FreeMedia Ltd.
Free media limited
mtaa wa Mkwepu na Makunganya, jengo la Bilicanas, gorofa ya kwanza, SLP 15261, Dar es salaam, Tanzania
simu +255-22-2126233  •  faksi +255-22-2126234  •  Selula  0713 296570