BARAZA jipya la mawaziri lililotangazwa na Rais Jakaya Kikwete juzi limeanza kufichukua masuala kadhaa yaliyojificha nyuma ya uteuzi huo uliopokewa kwa hisia tofauti na wananchi wa kada mbalimbali. Uteuzi huo umeonyesha dhamira ya wazi na ya kweli ya rais...
RAIS Jakaya Kikwete jana aliwaapisha mawaziri wake 47 aliowateua juzi, ikiwa ni miaka miwili na ushei tangu alipochaguliwa kuwa Rais wa Nne wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania. Ni jambo la heri kwamba, miaka miwili baada ya kuingia madarakani, Kikwete amepata fursa ya kuijenga upya serikali yake kwa kuchagua mawaziri wapya akianzia na waziri mkuu...
JANA baada ya Baraza la Mawaziri kuapishwa, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Joseph Mungai, alieleza kufurahishwa kwake na uteuzi wa aliyekuwa Naibu wake, Lawrence Masha, kuwa waziri kamili wa Wizara ya Mambo ya Ndani na Usalama wa Raia, zikiwa zimeunganishwa zilizokuwa Wizara ya Mambo ya Ndani na ya Usalama wa Raia...
MKAZI wa mkoani Tabora, Peter Komba, aliyeng’atwa na mbwa, ameilalamikia Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa kushindwa kumpatia matibabu, kwa maelezo ya kutokuwa na kibali kutoka kwa ofisa mifugo ...
NDEGE ndogo aina ya Cessina 172 Lims Rokert, namba 5H-FUN, imeanguka na kuua watu wawili na wengine wawili waliokuwemo ndani yake walijeruhiwa, wote ni raia wa kigeni...
MWANAMUZIKI mahiri wa muziki wa kizazi kipya, Banana Zorro, akiwa na bendi yake ya B Band, amewaahidi wapendanao, kuwapa burudani ya aina yake katika onyesho litalorindima Siku ya Wapendanao ‘Valentine’s Day’, Februari 14 kwenye Ukumbi wa Royal Village mkoani Dodoma...
MABINGWA watetezi wa soka Tanzania Bara, Simba, jana walishindwa kutamba mbele ya Manyema FC ya jijijini, baada ya kutoka suluhu ya bila kufungana katika mechi, iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam...